Saturday, February 19, 2011

JINSI YA KUTATUA MIGOGORO KATIKA VIKUNDI

Migogoro ni hali ya kutoelewana baina ya watu Fulani katika jamii fulani. Migogoro inatokea pale watu hao wanapotofautiana mawazo ili kufikia maamuzi Fulani.migogoro hutofatiana kulingana na jamii husika,wakati,sababu/chanzo,wahusika, n.k.

SABABU ZA MIGOGORO

• Ushirikishwaji hafifu katika upangaji na utekelezaji wa shughuli za pamoja katika jamii.
• Mawasiliano duni hasa katika masuala muhimu yanoyoigusasehemu kubwa ya jamii.
• Mbinu dhaifu na zisizoendelevu juu ya utatuzi wa migogoro.
• Tabia ya kutokuwepo kwa ukweli na uwazi ambayo upelekea kutoaminiana ndani ya vikundi.
• Mahusiano ambayo hayana uwiano baina ya wadau katika shughuli za kijamii.
• Kutojiamini
• Kuwa na miundo dhaifu ya uongozi na taratibu wa kuendesha shughuli za vikundi.
• Vikundi kutokuwa na mipango ambayo haitekelezeki.
• Kuwa na katiba au miongozo yenye mianya ambayo hutumiwa vibaya na baadhi ya wanakikundi.
• Utunzaji mbovu wa kumbukumbu.
• Wanakikundi kutoheshimu na kufuata taratibu au sheria katika uendeshaji wa shughuli za vikundi.
• Baadhi ya vikundi au jumuiya kuundwa kwa shinikizo bila ya mvuto wa wanakikundi.

ATHARI ZA MIGOGORO

• Kusambaratika kwa umoja / ushirikiano katika vikundi,
• Huduma na shughuli za maendeleo kuathilika.
• Ugomvi baina ya wanavikundi,
• Migomo ambayo wakati mingine hupelekea maandamano,

WAHUSIKA WA MIGOGORO
Wahusika wa migogoro wanatofautiana kulingana na aina ya mgogoro husika.katika migogoro ya vikundi wahusika wanaweza kuwa:-
• Viongozi,
• Wanakikundi
• Serikali,mfano viongozi wa serikari za mtaa
• Wafadhili,



MIKAKATI AU NJIA ZINAZOTUMIKA KUTATUA MIGOGORO
• Kuongeza kiwango cha ushirikishwaji wa wanakikundi
• Kupelekea uamuzi kwa njia ya mazungumzo kama mbinu ya kupata suluhu endelevu
• Kujenga uwezo wa ndani wa kutatua migogoro.
• Adhabu zinazotolewa hulenga kufundisha na siyo kukomoa au kuleta chuki na mgawanyiko unaoweza kutokea kutokana na hatua hizo.
• Kutoa mafunzo kwa vikundi husika katika njia za kutatua migogoro, mafunzo pia yanaweza kutumika kama kinga ya kupunguza mifumuko ya migogoro mingine.
• Kuboresha mawasiliano katika vikundi.
• Kutoshinikiza maamuzi yoyote yale.
• Kuhakiki sifa za watu waoomba unakikundi
• Mikutano na vikao vya kikundi ifanyike kwa wakati unaokubalika kikatiba.

Thursday, February 17, 2011

KILIMO CHA NYANYA KAHE


Shamba lililooteshwa nyanya.


Mwanakikundi wa FASO ndugu,Kimati akiwa na mtoto wake katika shamba lao la umwagiliaji.

Mashine ya petroli inayotumiwa na wakulima wadogo katika kilimo cha umwagiliaji.

KILIMO CHA NYANYA KAHE


Nyanya zikiwa zimestawi vizuri katika moja ya shamba la mwanakikundi wa FASO.