Thursday, August 16, 2012

ROMANA MAKATA A STRONG WOMEN IN MOSHI.

FASO through a WED Program- Women Empowerment Development visited a strong women at Majengo street here in Moshi munispal. Romana is a aged women about 50 years who living with HIV. She is a widow, living in her own house at majengo street in moshi, a mudhouse but she trying to moderate her house by building a block house outside her mady house.

A women is an entrepreneur who practice horticulture, livestoking, cloth making 'Batiki'  and also she doing a food processing through drying. 'My source of income is through this activities and i built this house, paying fees for my child studying university, i used to get credits from majengo VICOBA and other financial institutions which help to increase my capital and sending my childrens and groundchildren to school and university '- she said.

'I need a support from government, non-goverment, individual and companies to help me so as i can live a better life through entreprenuership'

Romana in her trees plantation.

Romana show animal food she used to process

She is also a craftwomen

Romana show her chickens


She also selling a wood for source of power

She also doing urban farming

This is a house she build

A block house she build outside with a mudhouse in side she living.


She also packaging a medical seeds

Apart from that Roman own her registered enterprise called ADERMANA ENTERPRISES dealing with Batic processing and Handcraft. If you  want to contact with her just call her direct through phone number
+255 755 752 504 or contact as for more details.

Sunday, August 12, 2012

SHIRIKA LA FASO LAFANYA SEMINA YA KILIMO KWA VIJANA KATIKA KATA YA KAHE,MOSHI VIJIJINI.

 Shirika lisilo la kiserikari la Fumbuka Agro Solution Organization (FASO) limefanya semina ya kilimo kwa vijana wa kata ya kahe moshi vijijini siku ya jumamosi, tarehe 11/08/2012. Katika semina hiyo jumla ya vijana therathini (30) kutoka vijiji 6 (kila kijiji vijana 5), vijiji hivyo ni Ngasinyi,Oria,Mawalla,Mwangaria,Kisangesangeni na Rau waliudhulia semina hiyo ya mafunzo. Akizindua semina hiyo Diwani wa kata ya Kahe Mh.Aminiel Kimati amewataka vijana kufanya kazi na kuwa wavumilivu kusubili mafanikio bila kuwa na haraka. Diwani huyo amewataka vijana waudhulie katika semina mbalimbali za maendeleo na waache tabia ya kudai posho katika semina hizo kwani semina hizo ni kwa ajili ya maendeleo yao.

Afisa kilimo na mifugo wa kata ya Kahe Bw.Lekule amewataka vijana hao kufanya kitu cha ziada baada ya semina hiyo badala ya kusikiliza na kuacha mambo hayo waliyojifunza yaishie hewani. Mkufunzi wa semina hiyo Mwl.Mushi kutoka chuo cha Kilimo na Mifugo Mwangaria aliwafundisha vijana hao jinsi ya kuchagua mazao bora kulingana na hali ya hewa ya ukanda wao. Vile vile mkufunzi huyo aliwafundisha vijana hao jinsi ya kuchagua pembejeo bora za kilimo kama mbegu, mbolea na madawa ya kuulia wadudu.

Mkurugenzi wa FASO Bw.Innocent Mbele na Meneja miradi Ndg. Moringe Allayana kwa pamoja wamewataka vijana hao kuzingatia mbinu bora za kilimo na kuacha kulima kwa mazoea. Vilevile watendaji hao wa shirika la FASO wamewataka vijana hao wajiunge katika vikundi ili wafanye kazi kwa pamoja na kunufaika na fursa mbalimbali.

Washiriki wa semina hiyo wameonyesha kufurahishwa kwa kufanyika kwa semina hiyo na wameliomba shirika la FASO kuandaa semina nyingine kama hiyo katika kata ya kahe na vitongoji vyake.


Afisa Maendeleo ya jamii kata ya kahe akimkaribisha mgeni rasmi.



Diwani wa kata ya Kahe, Mh. Aminiel Kimati (aliyesimama) akifungua semina hiyo.

 Afisa Kilimo na Mifugo Kata ya Kahe, Ndg.Lekule akiongea na wananchi.
Mwl. Mushi kutoka chuo cha Mwangaria akitoa elimu ya kilimo kwa vijana.

Mwl. Mushi akifundisha vijana.

Meneja miradi ya FASO, Ndg Moringe Allayana (kulia) na wanasemina wakifuatilia kwa makini.

Mwl.Mushi na Bw.Lekule wote kwa pamoja wakisisitiza jambo.

 Kijana wa Kahe akiuliza swali katika semina hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa FASO, Bw.Mbele akinukuhu mambo mbalimbali katika semina hiyo.

Vijana wakifuatilia kwa makini semina hiyo.


Mkurugenzi mtendaji wa FASO, Bw.Mbele (aliyechuchumaa mwisho kulia) akiwa na wana semina.

 Meneja miradi ya FASO, Bw. Moringe Allayana (aliyechuchumaa mwisho kulia) akiwa na wanasemina
Afisa Kilimo wa kata ya kahe Ndg Lekule (kushoto), Kijana wa Kahe, Mwl. Mushi na Bw.Mbele (kulia)wakiwa katika picha ya pamoja

Friday, August 3, 2012

FASO YATEMBELEA CHUO CHA KILIMO NA UFUGAJI MWANGARIA.

 Katika harakati zake za kupunguza umaskini kwa kuimiza kilimo na ujasiriamali, shirika la FASO limetembelea chuo cha kilimo na ufugaji cha MWANGARIA kilichopo kata ya KAHE,Moshi Tanzania.Lengo la ziara hiyo lilikuwa kujenga mahusiano kati ya shirika la FASO na chuo hicho. Mahusiano hayo yamezaa matunda kwa kuanza kuandaa semina ya mafunzo kwa vijana katika kata ya KAHE.

Meneja miradi ya FASO, Ndg .Moringe akipeana mkono na mkuu wa chuo hicho, Mzee Ngitiama

Mkurugenzi mtendaji wa FASO,Bw.Mbele akipeana mkono na mkuu wa chuo hicho cha kilimo, Mzee Ngitiama.

Baadhi ya madarasa ya chuo hicho.